RC Paul Makonda kuongea na vyombo vya habari dodoma leo je waandishi wameshasitisha maazimio yao waliyoyatoa
RC PAUL MAKONDA KUONGEA NA VYOMBO VYA HABARI
Waandishi wa habari wakiwa katika ukumbi tayari wakimsubilia mkuu wa mkoa Dar es salaam

Ikumbukwe kwamba hivi karibuni baada ya tukio lililoonekana ni la kuvamiwa kwa kituo cha habari cha clouds media na mkuu wa mkoa Dar es salaam RC Paul Makonda, waziri aliyekuwa akihudumu katika wizara hiyo aliunda kamati ya uchunguzi wa tukio hilo na kuja na mapendekezo kadhaa
moja ya mapendekezo hayo ni kutoandika habari zinazomhusu mkuu huyo wa mkoa wa Dar es salaam
Katika hali iliyozusha sintofahamu inasadikika ni kwa tukio hilo ndilo lililosababisha aliyekuwa waziri wa habari sanaa michezo na wasanii atolewe katika nafasi yake
lakini ni je baada ya hayo yote imekuwaje waandishi wakae mkao wa kula wakimsubilia mkuu huyo awape neno,
je ? ni kweli waandishi walitoa mapendekezo yale kwa umoja wao au yalikuwa mapendekezo ya mmoja wao tu, au baadhi ya vyombo vichache
Ila ukweli ni kwamba makonda leo anatarajiwa kuongea na vyombo vya habari , ataongea mambo mengi kumhusu na wananchi na vyombo vya habari vinashahuku ya kusikia kutoka kwake RC Paul Makonda
kila la kheri tukutane baadaye kidogo nikujuze kaongea nini
tutembelee tena www.wabongowatz.blogspot.com
Maoni
Chapisha Maoni